Thursday, March 24, 2016

STERLING HATARINI KUKOSA MSIMU ULIOBAKIA.

WINGA wa Manchester City, Raheem Sterling anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki sita mpaka nane kufuatia majeruhi ya nyonga yanayomsumbua, hivyo kumaanisha kuwa anaweza asicheze tena msimu huu. Kama akikaa nje kwa wiki nane inaanisha Sterling anaweza kurejea baada ya siku ya mwisho ya msimu wa Ligi Kuu Mei 15 lakini kabla ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ambayo itapigwa Mei 28. Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson amedai watakuwa wakifuatia maendeleo ya mchezaji huyo kama ataweza kucheza katika michuano ya Euro 2016. Kikosi cha Uingereza kinatarajiwa kutangazwa Mei 12 na Hodgson atakuwa na mpaka mwisho wa mwezi kabla ya kutangaza kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 kwa ajili ya michuao hiyo.

No comments:

Post a Comment