Thursday, March 24, 2016

WEST HAM KUONGEZA UWANJA WA OLIMPIKI.

KLABU ya West Ham United imethibitisha kuwa wanatarajia kuongeza vito 6,000 katika uwanja wao wa Olimpiki ili vifikie 60,000. Mahitaji ya tiketi kwa msimu yameongezeka katika klabu hiyo ambayo inashikilia nafasi ya tano katika msimamo wa Ligi Kuu msimu huu. Kutokana na hilo, klabu hiyo imedai kufanya mazungumzo na wabia wenzao katika uwanja huo ili waweze kuongeza viti. Makamu mwenyekiti wa West Ham, Karren Brady amesema wamefurahi kwani hatua waliyopiga ni kubwa na ni matumaini yao wataweza kutimiza malengo yao.

No comments:

Post a Comment