Monday, March 21, 2016

USHINDI WAMPA JEURI VAN GAAL.

MENEJA wa Manchester United, Louis van Gaal amesema matumaini yao ya kumaliza katika nne za juu yangekuwa yamefutika kama wangefungwa na Manchester city lakini anaamini sasa wana nafasi kubwa ya kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Bao pekee lililofungwa na chipukizi Marcus Rashford lilitosha kuipa United ushindi wa bao 1-0 dhidi ya mahasimu wao City jana. United kwasasa wako nafasi ya sita katika msimamo wa Ligi Kuu lakini wako nyuma ya City wanaoshika nafasi ya nne kwa alama moja. Akihojiwa Van Gaal amesema pengo hilo linegkuwa kubwa kama wangetoa sare au kufungwa lakini kwa ushindi waliopa anadhani sasa wana nafasi kubwa ya kufuzu michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment