Monday, March 21, 2016

ZIDANE ATAMBA KUWA YUKO TAYARI KWA CLASICO.

MENEJA wa Real Madrid, Zinedine Zidane amedai kuwa kikosi chake kimeonyesha kuwa kiko tayari kwa ajili ya mchezo wa Clasico kufuatia ushindi mnono wa mabao 4-0 waliopata dhidi ya Sevilla. Mabao ya Karim Benzema, Cristiano Ronaldo, Gareth Bale na James Rodriguez yalitosha kuifanya Madrid kubakisha alama moja kuifikia Atletico Madrid iliyoko nafasi ya pili katika msimamo wa La Liga baada ya nijana hao wa Diego Simeone kutandikwa na Sporting Gijon. Mchezo wa kwanza wa Madrid baada ya mapumziko kupisha mechi za kimataifa ni dhidi ya vinara wa ligi Barcelona ambapo watacheza katika Uwanja wa Camp Nou Aprili 2 na Zidane ana uhakika kikosi chake kiko tayari kwa ajili kutokana na kiwango bora walichoonyesha jana. Akihojiwa Zidane amesema amefurahishwa sana na mchezo huo kwani ni moja kati ya mechi walizocheza mechi walizocheza kwa kiwango kikubwa toka akabidhiwe mikoba ya kuinoa timu hiyo.

No comments:

Post a Comment