Monday, March 21, 2016

TUCHEL AIPONGEZA DORTMUND.

MENEJA wa Borussia Dortmund, Thomas Tuchel amekipongeza kikosi chake kwa uwezo mkubwa wlaiouonyesha katika ushindi waliopata dhidi ya Augsburg jana. Dortmund walitoka nyuma na kufanikiwa kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-1 katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa WWK Arena na kuongeza shinikizo kwa vinara wa Bundesliga Bayern Munich. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Tuchel amesema pamoja na kikosi chake kunza vibaya mchezo huo lakini walifanikiwa kujirudi na kucheza vyema baadae hatua ambalo ilisaidia kupata ushindi huo. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa sio mara zote timu inaweza kuanza kucheza vyema lakini jambo muhimu ni kuwa wlaipambana na kuhakikisha wanasawazisha bao na kutafuta mengine ya ushindi.

No comments:

Post a Comment