Monday, March 21, 2016

MARTINEZ AWAONYA WACHEZAJI WAKE.

MENEJA wa Everton, Roberto Martinez amewaonya wachezaji wake kuwa wanatakiwa kuimarika haraka kwani wanaweza kujikuta wakitolewa katika hatua ya nusu fainali ya Kombe la FA itakayofanyika katika Uwanja wa Wembley. Everton walipata nafasi hiyo kufuatia ushindi wa mabao 2-0 waliopata dhidi ya Chelsea, mabao ambayo yote yalifungwa na Romelu Lukaku Machi 12. Everton inatarajiwa kukabiliana na aidha Manchester United au West Ham United katika mchezo wao wa nusu fainali. Hata hivyo kufuatia kufungwa na Arsenal mabao 2-0 jana, Martinez ameonyesha wasiwasi na kuwataka wachezaji wake kusahau kipigo hicho haraka na kujiimarisha ili wasipoteze mchezo wao utakaofuata.

No comments:

Post a Comment