Monday, March 21, 2016

PIQUE AJITETEA.

BEKI wa Barcelona, Gerard Pique amepuuza taarifa zinazodai kuwa alistahili kutolewa nje katika mchezo waliotoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Villarreal jana. Barcelona walishindwa kulinda mabao yao mawili waliyopata awali kupitia kwa Ivan Rakitic na Neymar aliyefunga kwa penati baada ya Villarreal kurudisha mabao yote hayo na kulazimisha kugawana alama. Pique alilimwa kadi ya njano katika dakika ya 16 kwa kushika mpira na alirudia tukio hilo tena wakati akichuana na kiungo wa Villarreal Denis Suarez lakini hakupewa adhabu nyingine na mwamuzi. Akihojiwa Pique amesema kadi ya kwanza hakustahili kwani mpira ulimgonga kifuani na sio mkononi kama mwamuzi alivyoona hivyo hadhani kama alistahili.

No comments:

Post a Comment