Monday, March 28, 2016

WEST HAM KUMUWANIA IBRAHIMOVIC KIANGAZI.

KLABU ya West Ham United imethibitisha kutaka kumuwania Zlatan Ibrahomovic majira ya kiangazi lakini mmiliki mwenza wa timu hiyo David Sullivan hana uhakika kama Paris Saint-Germain watakuwa tayari kumuachia. Mshambuliaji huyo ambaye amefunga mabao 102 katika mechi 116 alizocheza Ligue 1, anatarajiwa kumaliza mkataba wake mwishoni mwa msimu huu na anategemewa kuondoka baada ya kushinda mataji manne katika kipindi miaka minne aliyokuwepo Ufaransa. Klabu za Ligi Kuu zimekuwa zikihusishwa kumuwania huku Ibrahimovic mwenyewe akielezea kuihusudu ligi hiyo na sasa West ham wamejitokeza hadharani kuonyesha kumuhitaji. Akihojiwa Sullivan amesema wana orodha ya karibu washambuliaji 10 kutoka sehemu mbalimbali Ulaya na fedha zao nyingi zaidi katika usajili zitakwenda kusajili mshambuliaji. Tajiri huyo aliendelea kudai kuwa anampenda Ibrahimovic na watajaribu kumsajili kama PSG wataamua kumuachia.

No comments:

Post a Comment