Monday, March 28, 2016

MOURINHO ADAIWA KUANZA MIKAKATI YA USAJILI MAN UNITED.

MENEJA wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho anadaiwa kuwa tayari ameshaanza mipango yake akiwa na Manchester United kama atachukua nafasi ya Louis van Gaal na anataka kusajili nyota watatu kwa mujibu wa jarida la Don Balon. Jarida la Hispania limedai kuwa Mourinho ameshaanza mipango ya usajili kwa kuweka wachezaji kadhaa nyota katika orodha yake akiwemo mshambuliaji wa Napoli Gonzalo Higuain, kiungo wa Real Madrid James Rodriguez na mshambuliaji wa Juventus Alvaro Morata. Mourinho ameshawahi kufanya kazi na Higuain wakati akiwa Madrid na United wameonyesha kuwa tayari ingawa watalazimika kulipa kitita cha paundi milioni 58 kwa ajili ya kumnasa nyota huyo wa kimataifa wa Argentina. United pia watakabiliwa na upinzani kwa Morata ingawa Madrid wako tayari kumnunua tena kama mkataba unavyotaka ili waje kumuuza kwa kiwango cha juu wakati Rodriguez yeye anatarajiwa kuondoka kiangazi kutokana na kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza.

No comments:

Post a Comment