Tuesday, April 19, 2016

ARDA TURAN AUGUA GHAFLA BARCELONA IKIIFUATA DEPORTIVO.

KLABU ya Barcelona inafuatilia kwa karibu afya ya Arda Turan kuelekea mchezo wao a kesho dhidi ya Deportivo La Coruna baada ya kiungo huyo kuugua ghafla. Arda alikosa mazoezi ya kikosi cha Barcelona leo kutokana na kuugua na atafanyiwa vipimo kesho asubuhi kabla ya mchezo huo.  Barcelona ilithibitisha taarifa hizo na kudai kuwa wataweza kumtumia hapo kama akipewa ruhusa na madaktari baada ya kuridhishwa na maendeleo ya afya yake. Barcelona wanaonolewa na Luis Enrique watakuwa wakijaribu kubadili matokeo katika mchezo huo baada ya kupoteza mechi zao nne zilizopita hali ambalo inatishia mbio zao za kutetea taji la La Liga.

No comments:

Post a Comment