Tuesday, April 19, 2016

VARDY HUENDA AKAADHIBIWA ZAIDI NA FA.

MSHAMBULIAJI wa Leicester City, Jamie Vardy huenda akakabiliwa na adhabu zaidi baada ya kushitakiwa na Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwa makosa ya kinidhamu. Vardy mwenye umri wa miaka 29, alizozana na mwamuzi Jon Moss baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu katika mchezo wa Jumapili iliyopita mabao walitoa sare ya mabao 2-2 na West Ham United. FA pia imeishitaki Leicester kwa kushindwa kuwatuliza wachezaji wake baada ya West Ham kupata penati katika dakika ya 83 ya mchezo. Vardy na Leicester wamepewa mpaka Alhamisi hii wawe wamejibu tuhuma zinazowakabili kabla ya kuchukuliwa hatua zaidi.

No comments:

Post a Comment