Tuesday, April 19, 2016

VIDAL AMTAKA SANCHEZ BAYERN.

KIUNGO wa Bayern Munich, Arturo Vidal amedai ataunga mkono hatua zozote zitakazochuliwa na klabu hiyo kwa ajili ya kumuwnaia nyota wa Arsenal Alexis Sanchez. Wachezaji hao wanajuana vyema kutokana na majukumu ya kimataifa wakiwa katika kikosi cha Chile, na Sanchez amekuwa akihusishwa na tetesi za kuhamia Ujerumani mara kadhaa huku kocha ajaye Carlo Ancelotti akidaiwa kuwa shabiki wake mkubwa toka akiwa Barcelona. Akihojiwa kuhusiana na hilo, Vidal amesema amekuwa akicheza na Sanchez toka wakiwa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 hivyo itakuwa vyema akija kucheza naye tena katika ngazi ya klabu. Bayern inakaribia kunyakuwa taji la Bundesliga na Vidal mwenye umri wa miaka 28 anataka washinde mataji yote msimu huu kwa kuwa bado yako ndani ya uwezo wao.

No comments:

Post a Comment