Tuesday, April 19, 2016

USHINDI WAIPA JEURI SPURS.



MSHAMBULIAJI wa Tottenham Hotspurs, Harry Kane amewaonya Leicester City kuwa bado wako nyuma yao baada ya kupunguza pengo la alama na kubaki tano dhidi ya vinara hao wa Ligi Kuu. Spurs waliongeza shinikizo kwa Leicester baada ya kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Stoke City katika Uwanja wa Britania jana usiku. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Kane mwenye umri wa miaka 22, amesema bado wataendelea kuwafukizia Leicester mpaka mwisho. Nyota huyo ambaye alifunga mabao mawili jana na kufikisha jumla ya mabao 24 msimu huu, aliendelea kudai kuwa kama wakiendelea kucheza kama walivyocheza jana hadhani kama kuna itaweza kuwafunga.

No comments:

Post a Comment