Monday, April 18, 2016

YANGA, AZAM KUWEKA HISTORIA MPYA AFRIKA.

VILABU vinavyoshiri michuano ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho inayoandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika-CAF, zinatarajiwa kuweka historia mpya kwa kucheza kwa mara ya kwanza mechi zao katikati ya wiki. Mechi za michuano hiyo mara nyingi zilizoeleka kuchezwa mwishoni mwa wiki lakini CAF sasa wameamua kubadilisha na kuchezwa katika siku ya Jumanne na Jumatano kutokana na maombi mengi yaliyotolewa kwao. Katika taarifa yake CAF imedai kuwa wamekuwa wakipata maombi mengi za mechi za michuano hiyo kuchezwa katikati ya wiki ili kutovuruga ratiba za mechi zao za ligi mwishoni mwa wiki. Timu za Tanzania, Yanga iliyopo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Azam iliyopo Kombe la Shirikisho zinatarajiwa kuwepo uwanjani katikati wiki hii kucheza mechi zao za mkondo wa pili. Yanga wao wataifuata Al Ahly jijini Cairo baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika Uwanja wa Taifa huku Azam wao wakielekea Tunisia kuifuata Esperance baada ya kuibuka kidedea kwa kushinda mabao 2-1 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Uwanja wa Chamazi.

No comments:

Post a Comment