Monday, April 11, 2016

CHINA YABAINISHA MIPANGO YAKE YA KUJA KUWA SUPER POWER KWENYE SOKA.

TAIFA la China limezindua mikakati yake ya kuja kuwa taifa lenye nguvu kisoka ifikapo mwaka 2050, kwa mipango ya kupata vijana wadogo na wakubwa zaidi ya milioni 50 wachezaji soka ifikapo mwaka 2020. Malengo mengine yanajumuisha kuwa na walau vituo vya soka 20,000 kwa ajili ya mazoezi na viwanja 70,000 ifikapo mwaka 2020. Wakati China ikifanya vyema katika michuano ya Olimpiki na Paralimpiki, taifa hilo limefanikiwa kufuzu mara moja pekee katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2002. Rais wa China Xi Jinping ameonyesha kuwa na shauku kubwa katika soka ambapo mara kadhaa amekuwa akikaririwa akidai kuwa anataka taifa hilo kutwaa Kombe la Dunia katika kipindi cha miaka 15 ijayo.

No comments:

Post a Comment