Monday, April 11, 2016

KOMPANY MAJANGA TENA.

NAHODHA wa Manchester City, Vincent Kompany hatarajiwi kuwepo katika mchezo wa marudiano wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kesho dhidi ya Paris Saint-Germain, kutokana na majeruhi. Meneja wa City Manuel Pellegrini amesema Kompany hayuko fiti asilimia 100 hivyo haitawezekana kumtumia. Beki huyo mwenye umri wa miaka 30, hajacheza mechi yeyote toka alipoumia katika sare ya bila kufungana waliyopata dhidi ya Dynamo Kiev. City na mabingwa Ufaransa PSG walitoka sare ya mabao 2-2 katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliochezwa jijini Paris wiki iliyopita.

No comments:

Post a Comment