Monday, April 11, 2016

RAFINHA KUWAKOSA ATLETICO.

KLABU ya Barcelona inatarajia kukosa huduma ya Rafinha katika mchezo wa marudiano wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Atletico Madrid, kutokana na majeruhi yanayomsumbua. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil alirejea hivi karibuni baada ya kukaa nje kwa miezi saba kufuatia kuumia goti, alicheza dakika 26 katika mchezo Barcelona walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Atletico wiki iliyopita kabla ya kuanza katika mchezo wa Jumamosi iliyopita waliofungwa bao 1-0 dhidi ya Real Sociedad. Rafinha alimpisha Andres Iniesta wakati wa mapumziko na sasa Barcelona wametangaza kuwa nyota huyo alipata matatizo ya msuli ambayo yatamuweka nje kwa muda. Katika taarifa ya klabu hiyo iliyotumwa katika mtandao wake imedai kuwa kurejea kwake uwanjani kutategemea jinsi gani atavyopona haraka.

No comments:

Post a Comment