Tuesday, April 26, 2016

DAVID SILVA KUIKOSA MADRID KATIKA MARUDIANO.

KIUNGO wa Manchester City, David Silva anatarajiwa kukosa mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania alipata majeruhi ya msuli wa paja katika kipindi cha kwanza cha mchezo wa jana ambao ulimalizika kwa sare ya bila kufungana. Na Pellegrini amebainisha kuwa hadhani kama kiungo hiyo anaweza kupona kwa wakati kabla ya mchezo wao wa wiki ijayo. Akihojiwa Pellegrini amesema Silva amepata majeruhi na hadhani kama atakuwa fiti ndani ya wiki moja.

No comments:

Post a Comment