Tuesday, April 26, 2016

DELE ALLI AINGIA MATATANI.

KIUNGO wa Tottenham Hotspurs, Dele Alli anaweza kukosa mechi zilizobakia msimu huu baada ya kushitakiwa kwa utovu wa nidhamu na Chama cha Soka cha Uingereza-FA. Hatua hiyo inakuja kufuatia picha cha video kuonyesha Alli akimpiga ngumi Claudio Yacob katika mchezo wao dhidi ya West Bromwich Albion juzi. Tukio hilo halikujumuisha katika taarifa ya mwamuzi wa mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1. Matukio kama hayo ya utovu wa nidhamu adhabu yake ni kufungiwa mechi tatu, hivyo kama chipukizi hiyo atakutwa na hatia anaweza kukosa mechi zote tatu za Spurs zilizobakia msimu huu. Alli ambaye alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwaka na Chama cha Wachezaji Kulipwa-PFA Jumapili iliyopita, amepewa mpaka baadae leo awe amejibu tuhuma hizo.

No comments:

Post a Comment