Tuesday, April 26, 2016

ARSENAL YAMUWANIA MSHAMBULIAJI WA CHELSEA.

KLABU ya Arsenal, inadaiwa kuwa na mipango ya kumuwania mshambuliaji wa Chelsea Dominic Solanke. Chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 18 yuko katika mzungumzo ya mkataba na Chelsea lakini anataka mkataba atakaolipwa paundi 50,000 kwa wiki. Lakini wakati Arsenal wakiwa hawataweza kufikia mshahara anaohitaji mshambuliaji huyo, wako tayari kumuhakikishia nafasi ya katika kikosi cha kwanza cha timu yao. Solanke ambaye mkataba wake unamalizika majira ya kiangazi, kwasasa yuko kwa mkopo katika klabu ya Vitesse ambako amefunga mabao saba katika mechi 24 alizocheza.

No comments:

Post a Comment