Tuesday, April 26, 2016

PELLEGRINI AANZA VISINGIZIO.

MENEJA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amedai Ligi Kuu imepuuza juhudi zao za kutaka mchezo wao wa Jumapili hii dhidi ya Southampton kusogezwa mbele ili wapate muda wa zaidi wa kujiandaa na mchezo wao wa marudiano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid. City na Madrid jana walitoka sare ya bila kufungana katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa michuano hiyo uliofanyika katika Uwanja wa Etihad na sasa wanakabiliwa na kibarua kizito pale watakapowafuata mabingwa hao wa kihistoria kule Santiago Bernabeu. Akihojiwa Pellegrini amesema wenzao Madrid watakuwa na muda zaidi wa kujiandaa kwani watakuwa na mchezo wa La Liga dhidi ya Real Sociedad Jumamosi wakati wao watachea jumapili. Meneja huyo aliendelea kudai wamejitahidi kufanya kila wawezalo ili wabadilishiwe mchezo huo lakini imeshindana kutokana haki za matangazo ya moja kwa moja.

No comments:

Post a Comment