Tuesday, April 26, 2016

KOMPANY AWACHIMBA MKWALA MADRID.

NAHODHA wa Manchester City, Vincent Kompany amedai asingejisikia vyema kama angekuwa nafasi waliyopo Real Madrid kufuatia sare ya bila kufungana waliyopata jana katika mchezo wa nusu fainali ya mkondo wa kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Madrid wanaonolewa na Zinedine Zidane, walikuwa wakicheza kwa tahadhari kubwa bila uwepo wa nyota wao Cristiano Ronaldo, haswa baada ya kufungwa ugenini na Wolfsburg katika hatua ya robo fainali. Timu zote mbili zilipata tabu kutengeneza nafasi katika mchezo huo na zinatarajiwa kukutana tena katika Uwanja wa Santiago Bernabeu Jumatano ijayo kupigania nafasi ya kucheza fainali ya michuano hiyo. Akihojiwa Kompany amesema anategemea wao kupata mabao katika mchezo huo na kama hilo likiwezekana utakuwa mzuri. Kompany aliendelea kudai kuwa wanajivunia rekodi nzuri waliyonayo kwa mechi zao ugenini hivyo hadhani kama wapinzani wao wanapaswa kufurahia.

No comments:

Post a Comment