Monday, April 25, 2016

JUVENTUS WATWAA TAJI LA TANO MFULULIZO LA SERIE A.

KLABU ya Juventus, imetwaa taji la Serie A kwa msimu wa tano mfululizo baada ya Napoli kukubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya AS Roma jioni hii. Ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Fiorentina jana uliwafanya kulikaribia taji hilo, na kushindwa kupata ushindi wa Napoli kunamaanisha kuwa hakuna timu yeyote itakayoweza kuifikia Juventus kwasasa. Msimu huu haukuwa rahisi kwa Juventus kwani Octoba 28 mwaka jana walikuwa wako katika nafasi ya 12 katika msimamo wa ligi wakiwa nyuma ya alama 11 kufikia kileleni. Hata hivyo mambo yalianza kuwaendelea vyema na kujikuta wakishinda mechi 24 kati ya 25 walizocheza toka wakati huo.

No comments:

Post a Comment