Monday, April 25, 2016

MESSI ATIMIZA AHADI YAKE KWA STEPHEN CURRY.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Lionel Messi ametoa ahadi yake kwa kumtumia Stephen Curry jezi yake yenye namba 10 mgongoni baada ya nyota huyo wa kikapu wa timu ya Golden State Warriors kufikisha mashabiki milioni 10 wanaomfuatilia katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram. Desemba mwaka jana, Messi alipokea fulana ya Warriors kutoka kwa Curry wakati alipofikisha mashabiki milioni 30 wanaomfuatilia katika mtandao huo wa kijamii. Messi aliapa kulipa fadhila wakati Curry atakapofikisha mashabiki milioni 10 na amefanya hivyo kama alivyoahidi. Messi alituma video katika ukurasa wake wa Instagram akionyesha jezi yake aliyosaini ambayo alipanga kumtumia Curry huku akimpongeza kwa mafanikio aliyopata.

No comments:

Post a Comment