Monday, April 25, 2016

FAINALI YA KOMBE LA FA YAMPA KIBURI VAN GAAL.

MENEJA wa Manchester United, Louis van Gaal amesisitiza amefanya kazi nzuri kukijenga kikosi na kuongeza kuwa amekuwa akifanya kazi na wachezaji ambao hawana ubora anaotaka. United wako nafasi ya tano katika msimamo wa Ligi Kuu wakiwa wamebaki na mechi nne, huku wakiwa wamefuzu hatua ya fainali ya Kombe la FA baada ya kuichapa Everton mabao 2-1 katika Uwanja wa Wembley. Van Gaal amekuwa akilaumiwa mara kadhaa kutokana na kikosi chake kucheza chini ya kiwango hatua ambayo sasa meneja huyo Mholanzi anailaumu klabu kwa kukosa wachezaji wepesi na wabunifu. Akihojiwa Van Gaal amesema aliwahi kusema kila kitu huko nyuma kwamba siku zote amekuwa akifundisha wachezaji ambao ubora wao sio aliohitaji. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa kipindi chote cha msimu amekuwa akihangaika na majeruhi wengi katika kikosi chake cha kwanza jambo ambalo limewarudisha nyuma kwa kiasi fulani.

No comments:

Post a Comment