Monday, April 25, 2016

CHIELLINI KUENDELEA KUSOTA BENCHI.

BEKI wa Juventus, Giorgio Chiellini anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu zaidi baada ya kupata majeruhi mengine akiwa mazoezini. Katika taarifa iliyotolewa na klabu hiyo nyota huyo wa kimataifa wa Italia ambaye alikosa mchezo wa jana walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Fiorentina anatarajiwa kuwa nje kwa siku 15 hadi 20 baada ya kuumia goti lake la kulia. Chiellini mwenye umri wa miaka 31, amekuwa nje ya uwanja kwa zaidi ya miezi miwili msimu huu baada ya kuumia goti pamoja na paja. Juventus wanaweza kutawadhwa mabingwa wa Serie A kwa mara ya tano mfululizo leo kama Napoli wanaoshika nafasi ya pili wakishindwa kuichapa AS Roma.

No comments:

Post a Comment