Monday, April 25, 2016

ZABALETA ATAMBA KUIFUNGA MADRID.

KIUNGO wa Manchester City, Pablo Zabaleta anaamini kikosi chao kina nafasi ya kutinga fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuichapa Real Madrid kuliko kama wangekuwa wanacheza na Bayern Munich au Atletico Madrid. Madrid ambao wamefunga mabao 26 msimu huu katika michuano hiyo wanatarajia kukwaana na City baadaye leo katika Uwanja wa Etihad kwenye nusu fainali ya mkondo wa kwanza. Pamoja na kufunga mabao mengi katika kampeni zao, hata hivyo Madrid nao wamekuwa na tatizo katika safu yao ya ulinzi kwa wameruhusu mabao mengi pia na Zabaleta anaamini kwa aina yao ya mchezo wanaweza kuwatoa mabingwa hao wa kihistoria. Akihojiwa Zabaleta amesema timu zote tatu ni ngumu lakini anadhani wao kupangwa na Madrid ni afadhali kidogo kwani kuna baadhi ya vitu wanashabihiana.

No comments:

Post a Comment