Friday, April 29, 2016

KLOPP AIONYA VILLARREAL.



MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp ameionya Villarreal kuwa watakuwa tayari kwa ajili yao wakati watakapokutana tena katika mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Europa League katika Uwanja wa Anfield wiki ijayo. Liverpool walitandikwa bao 1-0 na Villarreal katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliofanyika jana baada ya Adrian kupata bao hilo pekee dakika ya 90 katika Uwanja wa El Madrigal. Akihojiwa Klopp amesema hiyo ilikuwa hatua ya kwanza na bahati mbaya wameteleza lakini hana shaka kuwa watakuwa tayari kukabiliana na wapinzani wao hao wiki ijayo. Klopp aliendelea kudai kuwa kwasasa wanakwenda kufanyia kazi baadhi ya vitu ili watakapokutana katika mchezo ujao wawe wameimarika zaidi.

No comments:

Post a Comment