Monday, May 2, 2016

XAVI AMKINGIA KIFUA MESSI.

KIUNGO wa zamani wa Barcelona, Xavi amemkingia kifua Lionel Messi akidai kuwa sio aina ya mchezaji anayedanganya pindi awapo uwanjani. Messi alituhumiwa kudanganya baada ya Filipe Luis kutolewa katika ushindi wa Barcelona dhidi ya Atletico Madrid Januari mwaka huu, huku Mbrazil huyo akidai baadae kuwa Messi anapewa kipaumbele maalumu na waamuzi. Hata hivyo, Xavi amemtetea Messi na ana uhakika kuwa Messi ana tabia za kipekee pindi anapokuwa uwanjani kulingana na wachezaji wengine. Xavi amesema Messi ni mzuri kwani siku zote amekuwa mkweli na hana tabia za kudanganya ili aweze kupata faulo pindi anapokuwa uwanjani.

No comments:

Post a Comment