Monday, May 2, 2016

MADRID WANAVYOMNYIMA RAHA PELLEGRINI.

MENEJA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amesema angeweza kufanya tena hivyo baada ya kutumia kikosi dhaifu katika mchezo wao dhidi ya Southampton, huku akijipanga kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Real Madrid Jumatano hii. Pellegrini alifanya mabadiliko nane katika kikosi chake alichokitumia katika mchezo wa nusu fainali ya mkondo wa kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumanne iliyopita waliopata sare ya bila kufungana na Madrid. Mabadiliko hayo yalimtokea puani Pellegrini kwani alijikuta walitandikwa mabao 4-2 na Southampton katika Uwanja wa St Mary. Akihojiwa pellegrini amesema kama wangeweza kucheza Jumamosi angeweza kutaka kikosi chake kamili lakini alifanya hivyo jana kwasababu kuna mchezo wa Jumatano ambao aliupa kipaumbele. Pellegrini aliwapumzisha baadhi ya nyota wake akiwemo Sergio Aguero, Kevin de Bruyne na Vincent Kompany lakini alimuanzisha chipukizi wa miaka 19 Kelechi Iheanacho katika mchezo huo na kufunga mabao mawili.

No comments:

Post a Comment