Friday, April 15, 2016

KLOPP AKISIFIA KIKOSI CHAKE.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp amesifu ari waliyokuwa nayo wachezaji wake na kudai kuwa walipambana kufa na kupona na kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Europa League. Liverpool walitoka nyuma wakiwa wameshafungw amabao 3-1 na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 4-3 jana dhidi ya Borussia Dortmund na kutinga hatua hiyo kwa jumla ya mabao 5-4. Akihojiwa Klopp amesema ni vigumu kuelezea ilivyokuwa kwani mchezo ulikuwa wa ajabu na ulikuwa usiku mzuri katika Uwanja wa Anfield. Mabao ya Liverpool katika mchezo huo yalifungwa na Divock Origi, Philippe Coutinho, Mamadou Sakho na Dejan Lovren huku yale ya Dortmund yakifungwa na Henri Mkhitaryan na Pierre-Emerick Aubameyang aliyefunga mawili. Klopp aliendelea kudai kuwa walistahili ushindi huo kwakuwa walitengeneza nafasi nyingi na kupambana na kama mashetani.

No comments:

Post a Comment