Friday, April 15, 2016

XAVI AIKUMBUKA BARCELONA.

NAHODHA wa zamani wa Barcelona, Xavi amesema amekumbuka maisha yake katika klabu hiyo baada ya kuondoka mwishoni mwa msimu uliopita. Xavi aliyetokea katika akademi maarufu ya klabu hiyo ya La Masia, aliondoka Camp Nou kiangazi mwaka jana baada ya kupita miaka 25 na kwenda klabu ya Al Sadd ya Qatar. Hata hivyo, baada ya kukaribia mwaka toka aondoke Hispania, Xavi amebainisha kuwa ameikumbuka Barcelona. Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 36, amesema anakumbuka zaidi hali inavyokuwa katika vyumba vya kubadilishia nguo na utani wanaofanyiana pamoja na kila kitu kuhusu klabu hiyo. Xavi pia amekiri anaweza kugeukia ukocha pindi atakapotundika daruga zake siku zijazo.

No comments:

Post a Comment