Friday, April 15, 2016

WENGER BADO AOTA UBINGWA WA LIGI KUU.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger haamini kama mbio za Ligi Kuu zimekwisha na kusisitiza kuwa wanapaswa kushinda kila mechi wakati shinikizo likiongezeka kwa wapinzani wao. Arsenal wako nyuma ya vinara Leicester City wakitofautiana kwa alama 13, lkini wakiwa na mchezo mmoja mkononi. Akihojiwa Wenger amekiri kuna shinikizo kubwa lakini zaidi kwa wpainzani wao hivyo wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha wanashinda kila mchezo wao na kuona hali itakavyokuwa huko mwisho. Arsenal wanatarajiwa kuvaana na Crystal Palace Jumapili hii huku Leicester wakipambana na West Ham United na Tottenham Hotspurs waoashika nafasi ya pili wakichuana na Stoke City Jumatatu ijayo.

No comments:

Post a Comment