Wednesday, April 20, 2016

NEUER AONGEZA MKATABA NA BAYERN.

KIPA wa Bayern Munich, Manuel Neuer amesaini mkataba mpya ambao utamuweka Allianz Arena mpaka mwaka 2021. Kipa huyo wa kimataifa wa Ujerumani alitua Bayern akitokea Schalke msimu wa 2011-2012 na toka wakati huo amekuwa akipata nafasi katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo. Taarifa za hivi karibuni zilikuwa zikidai kuwa Neuer anaweza kushawishika kuungana na Pep Guardiola katika klabu ya Manchester City msim ujao lakini sasa amezima tetesi hizo kwa kusaini mkataba mpya na mabingwa hao wa Ujerumani. Neuer sasa anakuwa amefuata nyayo za kina Jerome Boateng, Thomas Muller, David Alaba na Javi Martinez ambao nao wameongeza mikataba yao katika miezi ya karibuni.

No comments:

Post a Comment