Thursday, April 21, 2016

RATIBA YA KOMBE LA SHIRIKISHO; YANGA KWENDA ANGOLA.

KLABU ya soka ya Yanga imepangwa kucheza na klabu ya GD Esperanca ya Angola katika hatua ya mtoano ya timu 16 bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho. Yanga iliangukia katika michuano hiyo ambayo ni ya pili kwa ukubwa Afrika baada ya kufungwa na Al Ahly ya Misri kwa mabao 2-1 jana hivyo kuondolewa kwa jumla ya mabao 3-2 katika mechi mbili walizokutana. Katika hatua hiyo Yanga wanatarajiwa kuanzia nyumbani kabla ya kwenda ugenini ambapo mechi za mkondo wa kwanza zikitarajiwa kuchezwa Mei 6 na 8 huku zile za marudiano zikitarajiwa kuchezwa Mei 17 na 18. Baadhi ya mechi zingine zilizopangwa katika ratiba hiyo wababe wa Azam FC, Esperance ya Tunisia wao watavaana na MO Bejaia ya Algeria huku TP Mazembe waliovuliwa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika wao wakipangwa kucheza na Stade Gabesien ya Tunisia.

No comments:

Post a Comment