Friday, April 22, 2016

BERLUSCONI BADO AING'ANG'ANIA AC MILAN.

RAIS wa AC Milan, Silvio Berlusconi ameelezea uvumi uliozagaa kuhusu timu hiyo kununuliwa na kampuni kutoka China, akisisitiza ataiuza klabu hiyo pale tu atakapoona kuwa itakuwa katika mikono salama. Milan imekuwa katika mazungumzo na mfanyabiashara wa Thailand Bee Taechaubol ambaye amekubaliano yao ya awali ni kununua hisa asilimia 48 za klabu hiyo. Toka wakati huo kuna taarifa zimezagaa kuwa kampuni kutoka China inataka kuinunua klabu hiyo huku vyombo vya habari nchini Italia vikidai kuwa yuko tayari kutoa kitita cha euro milioni 700. Akihojiwa Berlusconi amekiri kuwa wataka kuu lakini kama mnunuzi sahihi atapatikana ili ajihakikishie kuwa anaiacha Milan katika mikono salama.

No comments:

Post a Comment