Friday, April 22, 2016

HODGSON KUMUACHA MPEMBA WA MAN UNITED.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson amesema atalazimika kumtoa sadaka mchezaji ambaye ana sababu nyingi zaidi za kuitwa ili aweze kumuongeza chipukizi Marcus Rashford katika kikosi chake kwa ajili ya michuano ya Euro 2016. Mshambuliaji huyo wa Manchester United mwenye umri wa miaka 18, amefunga mabao saba katika mechi 13 alizoichezea United toka alipopandishwa kikosi cha wakubwa Februari mwaka huu. Hodgson amekuwa akifurahishwa a chipukizi huyo lakini amesema kuna uwezekano mdogo wa kumchukua kwenda naye Ufaransa katika michuano hiyo. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa utakuwa uamuzi wa kijasiri kumjumuisha katika kikosi chake.

No comments:

Post a Comment