Friday, April 22, 2016

BAYERN KUWEKA HISTORIA BUNDESLIGA.

KLABU ya Bayern Munich inaweza kuweka historia Jumamosi hii kwa kutwaa taji la nne mfululizo la Bundesliga wakati watakaposafiri kwenda jijini Berlin kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Hertha Berlin. Ushindi katika mchezo huo utakaofanyika katika Uwanja wa Olimpiki utaifanya Bayern kujiimarisha kileleni kwa tofauti ya alama saba huku kukiwa kumebaki michezo saba huku wakiomba Borussia Dortmund wapoteza mchezo wao dhidi ya Stuttgart. Kama Dortmund akipoteza mchezo huo na Bayern kushinda hakuna shaka kuwa watatangazwa mabingwa kwani hakuna timu itakayoweza kufikia alama walizonazo. Kutwaa taji la Bundesliga mapema kutawapa ahueni katika mchezo wao utakaofuata wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano ijayo ambapo watasafiri kuifuata Atletico Madrid.

No comments:

Post a Comment