Friday, April 22, 2016

MARTINEZ ADAI HANA HOFU YA KUTIMULIWA EVERTON.

MENEJA wa Everton, Roberto Martinez amesema haofii mustakabali wake na kuwa kikosi chake kinapaswa kukabiliana na changamoto wanazokutana nazo. Everton ambao hawajapata ushindi katika mechi zao saba zilizopita, walitandikwa mabao 4-0 na Liverpool juzi, matokeo ambayo Martinez ameyaelezea kama mabaya. Klabu hiyo inakabiliw ana mchezo mwingine mgumu Jumamosi hii wakati watakapochuana na Manchester United katika Uwanja wa Wembley katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la FA. Akihojiwa Martinez amesema hana mpango wa kufuatilia watu wanasemaje kuhusu uwezo wake wa kuendelea kuinoa klabu hiyo kwani wana mambo muhimu ya kufanya. Meneja huyo aliongeza kuwa kwasasa wanafanyia kazi makosa ambayo yamekuwa aykijitokeza katika kikosi chao ili waweze kufanya vyema mechi zao zijazo.

No comments:

Post a Comment