Friday, April 22, 2016

HODGSON AMUHAKIKISHIA ROONEY SAFARI YA EURO.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson amemuhakikishia Wayne Rooney nafasi katika kikosi chake cha wachezaji 23 atakaowaita kwa ajili ya michuano ya Euro 2016 lakini alikataa kuhakikisha kama mshambuliaji huyo wa Manchester United atapata namba katika kikosi cha kwanza. Kutokana na kuwa na washambuliaji wengi wazuri wakiwemo wanaoongoza kwa ufungaji katika Ligi Kuu, Harry Kane mwenye mabao 24 na Jamie vardy mabao 22, Hodgson amesema Rooney anaweza kuachwa katika kikosi cha kwanza. Akihojiwa Hodgson amesema kwasasa ushindani ni mkubwa hivyo hawezi kumuhakikishia nahodha wake nafasi ingawa atamjumuisha katika kikosi chake. Uingereza itakabiliana na Urusi, Slovakia na Wales katika kundi B kwenye michuano hiyo ya timu 24 ambayo inatarajiwa kuanza Juni 10 nchini Ufaransa.

No comments:

Post a Comment