Friday, April 22, 2016

RONALDO HATIHATI KUIKOSA MAN CITY WIKI IJAYO.

KLABU ya Real Madrid imethibitisha kuwa Cristiano Ronaldo amepata majeruhi ya msuli wa paja, hivyo kuibua wasiwasi wa kutokuwepo katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester City wiki ijayo. Nyota huyo wa kimataifa wa ureno alitoka mwenyewe nje mwishoni mw amchezo dhidi ya Villarreal juzi huku akishikilia mguu wake wa kulia. Meneja wa Madrid Zinedine Zidane alidai kuwa hadhani kama majeruhi hayo yatakuwa mabaya wakati Ronaldo mwenyewe akiandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa instagram kuwa kila kitu kilikuwa kinaenda sawa baada ya tukio hilo. Hata hivyo, baada ya kufanyiwa vipimo imegundulika kuwa nyota huyo alipata majeruhi ya msuli na haijulikani ni kw amuda gani atakaa nje ya uwanja.

No comments:

Post a Comment