Thursday, April 28, 2016

OZIL AAMUA KUIHENYESHA ARSENAL.

KIUNGO wa Arsenal, Mesut Ozil amesema hana haraka ya kusaini mkataba mpya na anaweza kusubiri mpaka mwishoni mwa msimu kwa ajili ya mzungumzo na klabu. Ozil na Alexis Sanchez wote wamebakisha mikataba ya miaka miwili huku Arsenal wakiwa tayari kuwapa mikataba mirefu zaidi kipindi cha kiangazi. Lakini Ozil, ambaye tayari amevunja rekodi ya Ligi Kuu kwa kutoa pasi nyingi za kusaidia kwa msimu mmoja, alikaririwa katika mahojiano na redio moja nchini Ujerumani akidai kuwa hana haraka yeyote kusaini mkataba mpya. Ozil amesema bado ana mkataba wa miaka miwili hivyo ataona itavyokuwa pindi msimu utakapomalizika.

No comments:

Post a Comment