Thursday, April 28, 2016

DEL PIERO ATIA BARAKA ZAKE LEICESTER WACHUKUE UBINGWA.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Italia, Alessandro Del Piero ana matumaini Leicester City watatwaa taji la Ligi Kuu ili kuonyesha hakuna kinachoshindikana katika ulimwengu wa michezo. Leicester ambao wanadaiwa alama tatu pekee ili watwae taji hilo kwa mara ya kwanza, wanaongoza ligi kwa tofauti ya alama saba dhidi ya Tottenham Hotspurs wanaoshika nafasi ya pili. Msimu huu umekuwa wa kipekee kwao haswa kutokana na jinsi walivyohaha miezi 12 iliyopita wasishuke daraja. Ushujaa huo ulioonyeshwa na Leicester umewapelekea kujizolea mashabiki kutoka pmbe zote za dunia akiwa nguli wa Juventus Del Piero ambaye amewahi kucheza chini ya Claudio Ranieri wakati akiwa Turin. Del Piero amesema anependa Leicester watwae taji hilo kwasababu litakuwa jambo ambalo unaweza kuwaambia wajukuu kuwa hakuna kinachoshindikana katika michezo.

No comments:

Post a Comment