Thursday, April 28, 2016

PSG YAMTIA KITANZI CHIPUKIZI WA UFARANSA.

CHIPUKIZI wa kimataifa wa Ufaransa, Odsonne Edouardo amesaini mkataba wake wa kwanza kama mchezaji wa kulipwa na mabingwa wa Ligue 1 Paris Saint-Germain jana. Edouard alionyesha kiwnago kizuri katika michuano Ligi ya Vijana ya UEFA, akifunga mabao matatu na kusaidia mengine matatu katika mechi nane alizocheza na kufanya Laurent Blanc kumjumuisha katika kikosi chake kitakachopiga kambi kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao. Chipukizi huyo pia alionyesha kiwango bora katika michuano ya Ulaya kwa vijana chini ya umri wa maiak 17 mwaka jana ambapo alifunga mabao nane yakiwemo matatu aliyofunga katika mchezo wa fainali dhidi ya Ujerumani. Edouard mwenye umri wa miaka 18 alijiunga na akademi ya PSG mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment