Thursday, April 28, 2016

JUVENTUS WAMNG'ANG'ANIA POGBA.

KLABU ya Juventus inadaiwa kutokuwa na mpango wowote wa kumuuza kiungo wake Paul Pogba majira ya kiangazi. Klabu hiyo tayari imefanikiwa kutwaa taji lake la tano mfululizo la Serie A na sasa wako katika mipango ya usajili lakini kuuza wachezaji wake nyota haitakuwa sehemu ya malengo yao. Mkataba wa sasa wa nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa unatarajiwa kuisha mwaka 2019 na ofisa mkuu wa Juventus Beppe Marotta tayari ameshasisitiza Pogba ambaye ameshacheza mechi 175 toka atue Turin akitokea Manchester United, hatakwenda popote. Akihojiwa na radio moja nchini Italia mapema mwezi huu, Marotta amesema walishafanya maamuzi juu ya Pogba mwaka jana kuwa ataendelea kuwatumikia na mwenyewe anafurahia kuwepo hapo.

No comments:

Post a Comment