Thursday, April 28, 2016

SIMEONE ATAMBA BAADA YA KUIZABUA BAYERN.



MENEJA wa Atletico Madrid, Diego Simeone anadhani kikosi chake kilikaribia kufikia ubora wake kufuatia ushindi wa bao 1-0 waliopata dhidi ya Bayern Munich katika mchezo wa nusu fainali ya mkono wa kwanza ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya jana. Huku wakishabikiwa kwa nguvu na mashabiki wao katika Uwanja wa Vicente Calderon, Atletico walifanikiwa kupata bao hilo pekee katika dakika ya 11 kupitia kwa nyota wake Saul Niguez. Katika kipindi chote cha mchezo vijana wa Simeone walionyesha umahiri wao mkubwa katika kuzuia mashabulizi makali ya wapinzani wao ambao muda wote walikuwa langoni mwao. Akihojiwa kuhusiana na mchezo huo, Simeone aliwapongeza wachezaji wake kwa kiwango kikubwa walichoonyesha akidai walicheza sawa kama katika robo fainali walipokutana na Barcelona. Simeone aliongeza kuwa Bayern walikuwa na uwezo wa kubadili na hata kupata ushindi lakini bahati haikuwa upande wao kutokana na umahiri wa wachezaji wake.

No comments:

Post a Comment