Wednesday, May 25, 2016

LENS YAPIGA MARUFUKU MASHABIKI KULEWA MITAANI WAKATI EURO 2016.

MASHABIKI wa Uingereza na Wales hawataruhusiwa kunywa pombe katika mitaa ya jiji la Lens kabla na baada ya mchezo wao wa michuano ya Euro 2016 kwasababu amri ya saa 24 iliyotolewa. Mchezo huo utakaokuwa wa kundi B utafanyika katika mji huo siku ya Alhamisi ya Juni 16 mwaka huu. Siku ya mchezo huo polisi wa mji huo watakuwa wakikagua magari yanayoingia kuona kama yamebeba pombe. Mashabiki wasiokuwa na tiketi za mchezo huo au tiketi za eneo la mashabiki nje ya uwanja wameshauriwa kutosafiri kwenda Lens. Pombe zitaruhusiwa katika maeneo maalumu yaliyotengwa kwa ajili ya mashabiki na hatua hiyo imekuja ili kuimarisha zaidi ulinzi na amri itakuwa ikitekelezwa katika kila mchezo utakaofanyika kwenye mji huo wakati wote wa mashindano.

No comments:

Post a Comment