Wednesday, May 25, 2016

DANI ALVES AISHABIKIA ATLETICO.

BEKI wa Barcelona, Dani Alves amekiri kuwa angependelea zaidi Atletico Madrid washinde taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya badala ya mahasimu wao Real Madrid katika mchezo wa fainali unaotarajiwa kuchezwa Jumamosi hii. Atletico walio chini Diego Simeone ndio waliowang’oa mabingwa watetezi Barcelona katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kabla ya kuitoa tena Bayern Munich kwenye hatua ya nusu fainali. Madrid ndio timu pekee iliyopo mbele ya Atletico kwasasa ikiwa ni kama marudiano baada ya ile fainali ya mwaka 2014 ambapo Madrid waliibuka kidedea kwa kushinda mabao 4-1 katika muda wa nyongeza. Hata hivyo, Alves ana mawazo tofauti katika fainali hiyo itakayofanyika katika Uwanja wa San Siro jijini Milan, kwani anadhani Atletico wanastahili zaidi taji hilo kuliko Madrid. Alves amesema Atletico ni timu ambayo imepambana sana mpaka kufikia hapo walipo hivyo anadhani wanastahili taji hilo.

No comments:

Post a Comment