Wednesday, May 25, 2016

RANIERI ADAI MSIMU UJAO WATAPIGANIA KUBAKI LIGI KUU TU.

MENEJA wa Leicester City, Claudio Ranieri amedai kuwa lengo kubwa la kikosi chake msimu ujao litakuwa ni kubaki katika Ligi Kuu na sio kutetea taji lao. Leicester msimu uliopita walifanikiwa kuwashangaza wengi kwa kutwaa taji la ligi kwa mara ya kwanza katika historia yao huku wakimaliza kileleni kwa tofauti ya alama 10 dhidi ya Arsenal walioshika nafasi ya pili. Hatua hiyo inamaanisha kuwa Leicester msimu ujao watashiriki pia michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hivyo kuwaongezea majukumu kulinganisha nay ale waliyokuwa nayo msimu uliopita. Akihojiwa Ranieri amesema msimu ujao utakuwa msimu mwingine mzuri kwasababu ya ujio wa Pep Guardiola, Antonio Conte nap engine Jose Mourinho. Ranieri aliendelea kudai kuwa utakuwa msimu mzuri na mgumu lakini lengo lao kubwa halitakuwa kutetea taji lao bali kuhakikisha wanabaki katika Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment