Wednesday, May 25, 2016

PSG KUIPIGA BAO ARSENAL KWA KANTE.

KLABU ya Paris Saint-Germain inadaiwa kuipiga bao Arsenal katika mbio za kumuwania kiungo N’Golo Kante. Mabingwa hao wa Ufaransa walikutana na wawakilishi wa kiungo huyo mahiri wa Leicester City Aprili mwaka huu na toka wakati huo wamekuwa wakiendeleza na majadiliano huku wakiahidi kumuongeza mshahara wake. Kante ambaye mkataba wake unaweza kutenguliwa kwa kitita cha paundi milioni 20, alikata ofa ya mkataba mpya na kuna uwezekano mkubwa wa kuondoka Leicester kiangazi hiki. Arsenal bado inaonekana kuwa na nia ya kumnasa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 25 lakini tatizo dau lao linaweza kua dogo kulinganisha na PSG.

No comments:

Post a Comment